Friday, April 19, 2013

Tumechagua wenyewe!

Nataka nikiri kuwa sijawahi kupiga kura.Sijawahi kupiga kwasababu katika chaguzi zetu za demokrasia ya WENGI WAPE bila kujali uadilifu wao, si rahisi kupata kiongozi makini.Mimi naamini kama tunataka viongozi MAKINI basi lazima na wanaochagua wawe makini.Hatuwezi kupata viongozi makini daima ikiwa tunachagua kwa ushabiki wa vyama,rushwa na bila kuzingatia uadilifu wa WACHAGUZI.Tutabaki kuwaonyeshea kidole TUNAOWACHAGUA lakini vidole vinne vimetuelekea sisi TUNAOCHAGUA maana wasingekuwepo pale bila sisi KUWAWEKA PALE!

Kutoka kwa majirani